Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar Ali Haji Hassan amesema Baraza la Vijana Zanzibar lipo tayari kushirikiana na Taasisi binafsi zinazoshughulika na masuala ya Vijana kwa lengo la kuwasaidia Vijana wa kizanzibari kufikia malengo yao .
Ameyasema hayo huko ofisi ya Taasisi ya ZAFAYCO Mombasa kwa Mchina alipokuwa akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo inayoshughulika na masuala mbalimbali yanayowahusu Vijana.
Amesema ipo haja kwa Taasisi zisizo za Kiserekali kufanya kazi kwa karibu na Baraza la Vijana Zanzibar kutokana na mabaraza ya Vijana kuwepo shehia zote 388 za Zanzibar .
Akizungumzia lengo la Taasisi ya Baraza la Vijana Zanzibar ni kuwasaidia Vijana kufikia ndoto zao bila ya kujali tofauti zao za kisiasa, dini au Kabila.
Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya ZAFAYCO Abdullah Abeid amesema kupitia Taasisi anayoiongoza itashirikiana na Baraza la Vijana Zanzibar kuhakikisha wanamfikia kila kijana wa kizanzibari anapata huduma zinazotolewa na Taasisi hizo.
Akizungumzia huduma wanazozitoa katika Taasisi hiyo ni pamoja na masuala ya uchumi, siasa , afya na elimu.
